CHIVAVIRO NA YANGA
🚨 Dili la mshambuliaji Ranga Chivaviro kutua Yanga limeshatibuliwa baada ya klabu ya Kaizer Chiefs inayomalizana na Kocha Nabi kumalizana naye juu kwa juu fasta.
.
Chivaviro alikuwa anawindwa vikali na klabu mbili za Tanzania, Azam na Yanga lakini mabingwa hao wa Ligi Kuu ya Tanzania ndio waliokuwa wakiongoza mbio za kuwania saini yake.
.
Taarifa za Uhakika kutoka klabu yake ya zamani ya Marumo Gallants ni kwamba tayari mshambuliaji huyo alishasaini mkataba wa awali wa miaka miwili na klabu ya Kaizer Chiefs.

Comments
Post a Comment